Matangazo

HTML/JavaScript

Zijue dalili za mtu aliyeoa au kuelewa na jini bila yeye kujua

Zijue dalili za mtu aliyeoa au kuolewa na jini bila kujua

Majini wakiwa kama viumbe hai nao hutamani kuwa na mke au Mume wa kibinadam

Hali hii hupelekea kutafuta ampendaye ktk wanadam na kufunga nae ndoa hata bila binadam huyo kupenda.

Na hizi ni dalili za aliyeoa au kuolewa na jini

1. Hapendi kabisa kuwa karibu na wanaume/wanawake hususan kama haja oa, kwa kuwa tayari ana mume/mke wa kiroho

2. Akichumbiwa/akichumbia lazima aharibu uchumba
mwenyewe , lazima atabadilisha mawazo na kusema simtaki mwaume/mwanamke huyo tena, yule jini ndiye anamletea mawazo ya kukataa mwenyewe. Huyu ni JINI TWAYR {qarnail}.

3. Kama akikaribia kuolewa/kuoa lazima atakataa lakini baadaye umri ukienda anajisikia vibaya

4. Kama aking’anga’ana na kuolewa/kuowa hawezi kuifurahia ndoa yake kabisa ataona ndoa kama
ni mateso, vile vile hawezi kumpenda mume/mke wake kabisa ,

mumewe/mkewe akiwa mbali
anammiss akija anajisikia kumchukia kabisa, kumchukia mwenza wako pindi anapo kuwa karibu na wewe. Huyu ni JINI SUBIANI.

5. Kama ameolewa/kuowa hawezi kupata mtoto kwa maana Yule mume/mke anaona wivu kuona
mkewe/mumewe anazaa na mume/mke mwingine, Hata
kama akifanya biashara hawezi kufanikiwa kabisa kwa maana jini yule anammiliki.

6. Kua na hasira sana bila hata sababu za msingi

7. Kuwa na hali ya kutojali au kuthamini wengine umimi na kujiona wa thamani peke yake kuliko wengine.

8. Kuchukiwa na ndugu jamaa na marafiki anakufanya ufanye mambo yakuchukiza wengine

9. Kujiona mtu mwenye mikosi nuksi na balaa tupu

10. Kuvurugika kwa mipango/ mambo yako/ hasa ya maendeleo na kila unachopanga hushindikana hata kama ukisaidiwa na mwisho hujiona hufai

11. Kuumwa kichwa pindi wakat unasoma Qur'aan au Biblia

12. Kutokujisikia kuomba au kusinzia pindi unapotaka kuanza maombi, huishiwa nguvu
kabisa, Na kuishia kuhangaika kama mtu asiyejua lakufanya. Kwa hiyo inawezekana jini anapoanza kumfuata mtu na kufanya mapenzi naye, mtoto
anaweza kuzaliwa. Nje ni mtu lakini kwa ndani siyo mtu ni shetani na ndio  maana unajiona ni
wa ajabu ajabu, kuna wengine usiku unaota
amezaa watoto siyo kwamba umeota ni kweli umezaa watoto wa kijini, na wale wanaporudi ujinini wanakurudia na kukuletea wewe
matatizo.

No comments

Powered by Blogger.